Wednesday, 9 December 2015

SERIKALI YA WANAFUNZI YA CHUO CHA USTAWI WA JAMII - ISWOSO KWA KUSHIRIKIANA NA MENEJIMENT YA CHUO CHA USTAWI WA JAMII YAADHIMISHA SIKU YA UHURU KWA KUFANYA USAFI KATIKA MAENEO YA CHUO

Share it Please
Makamu wa rais wa serikali ya wanafunzi ISWOSO (wa tatu kutoka kushoto) akiwa na baadhi ya menejiment ya chuo cha ustawi wa jamii akiwemo mkuu wa idara ya Ustawi wa Jamii Leah Omari (wa tatu kutoka kulia), wakipozi baada ya kumaliza usafi wa maeneo ya chuo cha ustawi wa jamii, katika kuadhimisha miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kwa kufanya usafi wa mazingira, kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu.

Kufuatia agizo la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kutumia siku ya maadhimisho ya uhuru wa Tanzania,  ya kufanya usafi wa mazingira kwa ujumla ili kupambana na ugonjwa wa kipindupindu, serikali ya wanafunzi ya Taasisi ya Ustawi wa Jamii - ISWOSO ikiongozwa na makamu wa Rais wa serikali hiyo Mheshimiwa Stella Wadson, pamoja na menejiment ya chuo cha ustawi wa jamii, wameshiriki kufanya usafi huo katika maeneo mbalimbali ya chuo cha ustawi wa jamii.

Makamu wa Rais wa serikali ya wanafunzi -ISWOSO  (kushoto ) Mheshimiwa Stella Wadson akiwa na waziri wa elimu wa Mheshimiwa Mabena wakiendelea na zoezi la usafi wa mazingira katika maeneo ya chuo.

Baadhi ya viongozi wa serikali ya wanafunzi ISWOSO walioshiri katika zoezi la usafi wa mazingira katika chuo cha ustawi wa jamii. Kutoka kushoto ni waziri mkuu Mh. Bendera,  waziri wa elimu Mh. Mabena, waziri wa Miundombinu Mh. Nassary na naibu waziri wa fedha Mh. Peace Nnauye. 

Pichani ni waziri wa afya na mazingira wa serikali ya wanafunzi ISWOSO Mh. Anderson Mahundi  (kushoto), na Mh. Victor. 



Baadhi ya viongozi wa ISWOSO walioshiriki katika zoezi la usafi wa mazingira chuo cha ustawi wa jamii kufuatia agizo la rais wa Tanzania kuadhimisha siku ya Uhuru wa Tanzania kwa kufanya usafi wa mazingira kupambana na ugonjwa wa kipindupindu.


No comments:

Post a Comment

Followers

Check us on Facebook

Designed By WijasWillie | SharpMedia