Wednesday, 9 December 2015

NAIBU WAZIRI WA MAADILI - ISWOSO AONGOZA WANACHUO WANAOISHI HOSTEL YA TAASISI YA USTAWI WA JAMII KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA KATIKA MAENEO YANAYOZUNGUKA HOSTELI HIYO

Share it Please
Naibu waziri wa nidhamu na maadili wa serikali ya wanafunzi ya chuo cha ustawi wa jamii - ISWOSO Mheshimiwa Hajrat Munisy, amewaongoza wanachuo wanaoishi hosteli ya taasisi kwa kufanya usafi wa mazingira, katika kupambana na ugonjwa wa kipindupindu.

Naibu waziri wa nidhamu na maadili Mh. Hajrat Munisy (wa kwanza kushoto) akiwa na baadhi ya wanachuo wanaoishi hosteli ya taasisi ya ustawi wa jamii, wakiadhimisha siku ya uhuru wa Tanzania kwa kufanya usafi wa mazingira.

Hatua hiyo ni kutimiza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa John Pombe Maghufuli ya kuadhimisha miaka 54 ya uhuru wa Tanzania kwa mwaka huu, kwa kufanya usafi wa mazingira, ili kupambana na ugonjwa wa kipindupindu ulioenea kwa kasi katika mikoa mbalimbali hapa nchini.


Baadhi ya wanafunzi walijitokeza kwa wingi kufanya usafi wa mazingira yanayozunguka hosteli hiyo, kufuatia mwamko walioupata kutoka kwa viongozi wa serikali ya wanafunzi ISWOSO pamoja na menejiment ya uongozi wa chuo cha ustawi wa jamii.


Jengo la hostel wanaloishi wanachuo cha ustawi wa jamii, wakishiriki usafi kwa kuanzia vyumbani mwao na maeneo ya nje ya hosteli hiyo.

No comments:

Post a Comment

Followers

Check us on Facebook

Designed By WijasWillie | SharpMedia