Monday, 9 May 2016

MAADHIMISHO YA WIKI YA UJUZI (CAREER DAY) NDANI YA TAASISI YA USTAWI WA JAMII

Share it Please


Wizara ya elimu kupitia serikali ya wanafunzi ya chuo cha ustawi wa jamii – Institute of Social Work Students Organization  ISWOSO kwa kushirikiana na club za vitengo vinavyotoa taaluma chuoni hapa, wameandaa maadhimisho ya siku ya ujuzi maarufu kama CAREER DAY yenye lengo la kuwakutanisha wataalamu mbalimbali waliosoma chuoni hapo wa fani tofauti kuanzia leo tarehe 9 hadi 12 mwezi huu wa tano, 2016.

Maadhimisho hayo ya Career day yanashirikisha wataalamu na wanachuo kutoka taaluma ya Rasilimali watu (Human Resource Management), Mahusiano kazini (Industrial Relations) na Ustawi wa jamii (Social work).

Akifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Taifa – TBC mwishoni mwa wiki, waziri mkuu wa serikali ya wanafunzi ya chuo cha ustawi wa jamii mheshimiwa Maurice Bendera, amewaomba wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali kushiriki katika wiki hii kwani kuna mambo mengi ambayo yameandaliwa na wanachuo.

Ametaja baadhi ya mambo yatakayokuwa yakiendelea katika wiki hii ujuzi ni pamoja na Huduma ya unasihi (Counseling) ikayokuwa ikitolewa na wanachuo, elimu kwa upande wa labour studies kwani imeonekana wafanyakazi wengi hawafahamu sheria mbalimbali zinazowaongoza na ili kutambua haki zao kutoka kwa mwajiri, pamoja na maafisa rasilimali watu ambao watatoa elimu kuhusiana na sheria za kazi (Employment Labour Relations Act), na kuwakaribisha wanafunzi wote na jamii kwa ujumla kushiriki kikamilifu kwani huduma hii inatolewa bure.

Siku ya jumatano imetengwa rasmi kwa ajili ya semina kutoka kwa watu ambao wanafanya vizuri kwenye ujasiriamali ambapo itawahusu wanafunzi wa ngazi ya cheti, diploma na degree ambao ili kuwaandaa kukabiliana na soko la ajira pindi wanapomaliza masomo yao.
Kilele cha maadhimisho hayo ni siku ya alhamis ya tarehe 12 May, 2016 ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bi Samia Suluhu Hassan.

Wiki ya Ujuzi ndani ya Taasisi ya ustawi wa jamii, inaletwa kwenu kwa kushirikiana na wizara ya elimu kupitia ISWOSO, Social work club, Human Resource Club, Industrial Relations Club, PSPF na Brighter Monday Tanzania.

Nyote mnakaribishwa.


No comments:

Post a Comment

Followers

Check us on Facebook

Designed By WijasWillie | SharpMedia