Friday, 13 May 2016

PATA VIONJO - YALIYOJIRI KWENYE CAREER DAY USTAWI WA JAMII

Katika kunogesha maadhimisho ya siku ya ujuzi (Career day) yaliyofanyika jana alhamisi ya tarehe 12/05/2016, vikundi mbalimbali vya kitaaluma vilitoa burudani inayohusiana na kile wanachojifunza katika taaluma yao.

Kwa upande wa taaluma ya Social work, wanaharakati wa kikundi cha Protect Her 4 Life, chenye lengo la kupambana na kila aina ya ukatili wanaofanyiwa wanawake na wasichana, kilitoa igizo lililolenga namna ukatili unavyofanyika, ni kwa kiasi gani kutojielewa au kutojengewa uwezo kunavyosababisha mtu kutoweza kushiriki katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo, namna mwanamume anayomtupia lawama mke kwa kila tatizo linalomkuta mtoto na kuelimishwa kuwa naye anapaswa kuwa sehemu ya kutoa malezi bora kwa watoto.

Pia igizo hilo lilionesha ni kwa namna gani afisa ustawi wa jamii anavyoweza kufanya kazi na timu ya wataalamu wa fani mbalimbali, na katika igizo hili wameshirikiana na polisi kufanikisha mwanamume aliyefanya ukatili amekamatwa na kufikishwa dawati la jinsia, pia afisa ustawi wa jamii ameweza kushirikiana na mwalimu wa shule katika kusaidiana kutoa elimu ya afya ya uzazi kwa vijana hasa kipindi cha balehe ili kuepuka mimba wakiwa mashuleni na kuonesha ni kwa kiasi gani maafisa ustawi wa jamii wahahitajika mashuleni. Na pia kumjengea uwezo mwanamke afahamu haki zake na fursa mbalimbali za kimaendeleo.



Wanachuo wa fani ya ustawi wakijiandaa kwa igizo

Mwanamke aliyepigwa na mumewe akishauriwa kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi, kutokana na kipigo cha mara kwa mara anachokipata kwa mumewe.





Msoma risala kwa upande wa Industrial Relations wao hawakuwa na igizo.





Continue Reading...

Thursday, 12 May 2016

CAREER DAY 2016 YAFANA USTAWI WA JAMII


Kilele cha maadhimisho ya ujuzi (Career day) katika chuo cha ustawi wa jamii, kimehitimishwa leo katika viwanja vya chuo cha ustawi wa jamii – Dar es Salaam.



Baadhi ya wanachuo wa taaluma ya ustawi wa jamii waliohudhuria maadhimisho hayo


Baadhi ya wanachuo wa taaluma ya Industrial Relation waliohudhuria maadhimisho hayo


Baadhi ya wanachuo wa taaluma ya Human Resource waliohudhuria maadhimisho hayo


Akitoa salamu za ufunguzi, rais wa serikali ya wanafunzi chuo cha ustawi wa jamii Mheshimiwa Hemed Haroub, amebainisha kuwa siku hii inalenga kuwakutanisha pamoja wajuzi wa fani zinazotolewa katika chuo cha ustawi wa jamii, pamoja na wale walio katika ajira, katika kushea mambo mbalimbali, na pia kutoa mawazo ya fursa za ajira.


Mheshimiwa Hemed - rais wa serikali ya wanafunzi


Rais wa serikali ya wanafunzi Mheshimiwa Hemed Haroub (aliyesimama) akitambulisha meza kuu, wa kwanza kulia ni makamu wa rais wa serikali ya wanafunzi chuoni hapo Mheshimiwa Stella Wadson


Kilele cha maadhimisho hayo kimefana kwa wanachuo kuainisha shughuli mbalimbali zinazofanywa na taaluma zao kwa njia ya maelezo, maigizo na kupitia risala.







 Pichani juu ni wanachuo wa taaluma ya ustawi wa jamii, wakielezea mambo mambo mbalimbali wanayofundishwa katika taaluma hiyo na namna inavyowasaidia katika kufanya kazi mbalimbali za kijamii.




Pichani ni wanataaluma ya Industrial Relation wakielezea shughuli zinazotekelezwa na wanataaluma hiyo pamoja na process nzima inavyotakiwa kufuatwa wakati wa kufanya Mediation.




Hapa ni kwenye meza ya wanachuo wa taaluma ya rasilimali watu (Human Resource) nao wakielezea kile wanachokipata katika chuo cha ustawi wa jamii, pamoja na namna taaluma hiyo inavyofanya kazi kwenye soko la ajira.


Wawakilishi kutoka mashirika mbalimbali waliweza kuhudhuria katika career day ya ustawi wa jamii, kutoa changamoto mbalimbali zinazotokana na ajira na pia kutoa mwongozo wa namna ya kuchangamkia fursa mbalimbali za ajira.

Miongoni mwa mashirika na wadau waliohudhuria ni pamoja Brighter Monday, PSPF, Zoom Tanzania pamoja na wawakilishi wa vyuo mbalimbali kikiwemo chuo kikuu cha Dar es Salaam.


Mwakilishi kutoka Brighter Monday, akielezea fursa mbalimbali za ajira zinazopatikana endapo mtu atajiunga online ili kupata taarifa mbalimbali za nafasi za ajira hapa nchini, kutoka kwa mashirika mbalimbali.


Career day katika ustawi wa jamii imeandaliwa na wizara ya elimu kutoka serikali ya wanafunzi ISWOSO kwa kushirikiana vilabu vya kila taaluma itolewayo ambapo kwa upande wa Human Resource inafahamika kama IHUMRESA, Industrial Relations – IRESA na Social Work – SOWOC.
Waziri wa elimu katika serikali ya wanafunzi - ISWOSO Mheshimiwa Mabena, akihojiwa na chombo cha habari cha ITV, kuelezea lengo la career day.










 Pichani juu ni baadhi ya wanachuo waliohudhuria kwenye career day, iliyofanyika katika viwanja vya chuo cha ustawi wa jamii.

Maadhimisho ya career day hufanyika kila mwaka na kwa kipindi yamehusisha taaluma zote tatu zinazotolewa katika chuo cha ustawi wa jamii ambazo ni Social work, Human Resource, na Industrial Relations, lengo likiwa ni kuziweka pamoja na kuongeza ufanisi, kwani hata katika soko la ajira zinategemeana, tofauti na miaka ya nyuma ambapo kila taaluma ilikuwa inaadhisha kivyake.

Continue Reading...

Wednesday, 11 May 2016

SEMINA ELEKEZI YA KUWAUNGANISHA WANAFUNZI KATIKA FURSA MBALIMBALI ZA AJIRA


Rais wa serikali ya wanafunzi ya chuo cha ustawi wa jamii – ISWOSO Mheshimiwa Hemed Haroub, amewataka wanachuo kuchangamkia fursa mbalimbali za ajira, ambazo zimewafikia katika chuo cha ustawi wa jamii hii leo.

Rais wa serikali ya wanafunzi - ISWOSO Mheshimiwa Hemed Haroub, akitoa hotuba fupi ya ufunguzi wa semina hiyo.




Pichani ni baadhi ya wanachuo walioshiriki kwenye semina hiyo.




NB: KWA HABARI NA PICHA ZAIDI ENDELEA KUTEMBELEA BLOG HII

Continue Reading...

Tuesday, 10 May 2016

KUELEKEA KILELE CHA SIKU YA UJUZI, VIONGOZI WA SERIKALI YA WANAFUNZI ISWOSO WASHIRIKI KATIKA KUFANYA USAFI KWENYE MAENEO YA CHUO CHA USTAWI WA JAMII


Viongozi wa serikali ya wanafunzi ya chuo cha ustawi wa jamii – ISWOSO wameshiriki katika zoezi la kufanya usafi katika maeneo yanayozunguka chuo hicho, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya ujuzi chuoni hapo.

Pichani ni baadhi ya viongozi walioshiriki katika zoezi la usafi

Zoezi hilo la usafi limeongozwa na wizara ya afya na mazingira ya serikali ya wanafunzi, na kuwashirikisha pia viongozi wa klabu za wanafunzi chuoni hapo, ikiwemo klabu ya rasilimali watu (Human Resource), Mahusiano Kazini (Industrial Relations), na ya uswawi wa jamii (Social Work Club).



















Pichani juu ni baadhi ya viongozi walioshiriki katika zoezi la kufanya usafi, ikiwa ni mwendelezo wa maadhimisho ya siku ya ujuzi (Career day) ambayo kilele chake kinatarajiwa kuwa siku ya alhamis ya tarehe 12/05/2016 katika viwanja vya chuo cha ustawi wa jamii.

Siku ya kesho jumatano ya tarehe 11/05/2016, kutakuwa na semina elekezi kwa wanachuo wanaotarajiwa kumaliza masomo yao mapema mwezi wa nane mwaka huu, itakayofanyika katika chuo cha ustawi wa jamii.

Semina hiyo imeandaliwa na ISWOSO lengo likiwa ni kutoa fursa kwa wahitimu ngazi mbalimbali kupata mawazo ya namna ya kutambua fursa za ajira zilizopo, ambapo wawezeshaji ni kutoka mfuko wa Mafao wa PSPF, Forever Living, Brighter Monday pamoja na mhamasishaji Chris Mauki na inatarajiwa kuanza saa saba hadi saa kumi jioni.


Shukrani kwa wapiga picha wote na wote walioshiriki katika zoezi la usafi.



Continue Reading...

Monday, 9 May 2016

MAADHIMISHO YA WIKI YA UJUZI (CAREER DAY) NDANI YA TAASISI YA USTAWI WA JAMII



Wizara ya elimu kupitia serikali ya wanafunzi ya chuo cha ustawi wa jamii – Institute of Social Work Students Organization  ISWOSO kwa kushirikiana na club za vitengo vinavyotoa taaluma chuoni hapa, wameandaa maadhimisho ya siku ya ujuzi maarufu kama CAREER DAY yenye lengo la kuwakutanisha wataalamu mbalimbali waliosoma chuoni hapo wa fani tofauti kuanzia leo tarehe 9 hadi 12 mwezi huu wa tano, 2016.

Maadhimisho hayo ya Career day yanashirikisha wataalamu na wanachuo kutoka taaluma ya Rasilimali watu (Human Resource Management), Mahusiano kazini (Industrial Relations) na Ustawi wa jamii (Social work).

Akifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Taifa – TBC mwishoni mwa wiki, waziri mkuu wa serikali ya wanafunzi ya chuo cha ustawi wa jamii mheshimiwa Maurice Bendera, amewaomba wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali kushiriki katika wiki hii kwani kuna mambo mengi ambayo yameandaliwa na wanachuo.

Ametaja baadhi ya mambo yatakayokuwa yakiendelea katika wiki hii ujuzi ni pamoja na Huduma ya unasihi (Counseling) ikayokuwa ikitolewa na wanachuo, elimu kwa upande wa labour studies kwani imeonekana wafanyakazi wengi hawafahamu sheria mbalimbali zinazowaongoza na ili kutambua haki zao kutoka kwa mwajiri, pamoja na maafisa rasilimali watu ambao watatoa elimu kuhusiana na sheria za kazi (Employment Labour Relations Act), na kuwakaribisha wanafunzi wote na jamii kwa ujumla kushiriki kikamilifu kwani huduma hii inatolewa bure.

Siku ya jumatano imetengwa rasmi kwa ajili ya semina kutoka kwa watu ambao wanafanya vizuri kwenye ujasiriamali ambapo itawahusu wanafunzi wa ngazi ya cheti, diploma na degree ambao ili kuwaandaa kukabiliana na soko la ajira pindi wanapomaliza masomo yao.
Kilele cha maadhimisho hayo ni siku ya alhamis ya tarehe 12 May, 2016 ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bi Samia Suluhu Hassan.

Wiki ya Ujuzi ndani ya Taasisi ya ustawi wa jamii, inaletwa kwenu kwa kushirikiana na wizara ya elimu kupitia ISWOSO, Social work club, Human Resource Club, Industrial Relations Club, PSPF na Brighter Monday Tanzania.

Nyote mnakaribishwa.


Continue Reading...

Followers

Check us on Facebook

Designed By WijasWillie | SharpMedia