Friday, 22 January 2016

WAZIRI MKUU MHESHIMIWA KASSIM MAJALIWA - MGENI RASMI UFUNGUZI WA MASHINDANO YA VYUO VIKUU DAR ES SALAAM

Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mashindano shirikisho la vyuo vikuu mkoa wa Dar es salaam.

Mwenyekiti wa shirikisho hilo bwana Imani Matabula, amesema ufunguzi huo utafanyika katika viwanja vya chuo kikuu cha Dar es salaam, ambapo jumla ya vyuo 32 vimethibitisha kushiriki mashindano hayo.

Bwana Matabula amebainisha kuwa, shirikisho hilo limeandaa michezo ya aina tano ambayo ni mchezo wa mpira wa miguu (Football), mpira wa Pete (Netball), Volleyball, Basketball pamoja na mchezo wa kuogelea (Swimming).

Michezo hii inajumuisha vijana wa vyuo vikuu lengo likiwa ni kuwakutanisha vijana kutoka vyuo vikuu wenye vipaji tofauti tofauti kwa ajili ya kufahamiana na kurejesha fikra za wanavyuo katika mlengo mmoja ambao ulikuwa na milengo tofauti kabla ya uchaguzi mkuu wa nchi uliofanyika October 2015, na kurejesha amani na mshikamano kwa vijana wote.

Mashindano hayo yataanza kesho tarehe 23 January, 2016 ambapo yatazinduliwa saa kumi jioni huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Waziri mkuu wa nchini Mheshimiwa Kassim Majaliwa na kilele cha mashindano hayo ni January 30, 2016.


Continue Reading...

WANACHUO NA WAFANYAKAZI USTAWI WA JAMII WASHIRIKI KUCHANGIA DAMU SALAMA KWA AJILI YA KUSAIDIA WAGONJWA



Wanachuo wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii, pamoja na wafanyakazi wa Taasisi hiyo, leo wamejitokeza katika viunga vya eneo la Taasisi hiyo kuchangia damu salama kwa ajili ya kusaidia wagonjwa wenye uhitaji wa damu.

Naibu Waziri wa Afya na Mazingira katika serikali ya wanafunzi - ISWOSO Mheshimiwa Judith Mangowi, akiongoza zoezi  hilo kwa kuhamasisha wanachuo kushiriki  kuchangia damu salama.

Rais wa Serikali ya Wanafunzi Taasisi ya Ustawi wa Jamii - ISWOSO, Mheshimiwa Hemed Haroub, akiteta jambo na mmoja wa wafanyakazi wa Sinza Hospital waliofika kwa ajili ya kuendesha zoezi la uchangiaji na ukusanyaji damu salama katika Taasisi hiyo.




Zoezi la kukusanya damu salama limeendeshwa na Hospitali ya Sinza - Dar es salaam, lengo likiwa ni kuwasaidia ndugu zetu wagonjwa wenye uhitaji wa msaada huu.

ISWOSO, Sinza Hospital na Taasisi ya Ustawi wa Jamii, inatoa shukrani kwa wote waliojitokeza katika zoezi hilo.
Continue Reading...

Saturday, 9 January 2016

Continue Reading...

PETER MAYUNGA Rais wa serikali ya wanafunzi CBE - MWENYEKITI MPYA WA BARAZA LA SENATE -TAHLISO


 Hatimaye Mwenyekiti mpya atakayeongoza baraza la senate la Jamii ya Vyuo vya Elimu ya juu nchini - TAHLISO apatikana.


Mwenyekiti mpya wa baraza la seneti la TAHLISO akitaka shukran kwa wajumbe wa baraza hilo, baada ya kutangazwa mshindi wa nafasi hiyo.

Mwenyekiti huyo amepatikana baada ya uchaguzi wa mkuu uliofanyika katika ukumbi wa chuo cha ustawi wa jamii kurudiwa kwa mara ya pili na Mheshimiwa Mayunga kuongoza kwa asilimia 60.42 ya kura zote zilizopigwa dhidi ya Rais wa serikali ya wanafunzi Chuo cha Diplomasia Mheshimiwa Nice Munissy, aliyepata asilimia 39.58 ya kura zote.

Mheshimiwa Nice Munissy,  mwanamke pekee aliyejitokeza katika kinyang'anyiro cha nafasi ya uenyekiti wa baraza la seneti, akitaka shukrani kwa wajumbe wa baraza hilo, na kuahidi kutoa ushirikiano kwa uongozi wa baraza hilo.

Awali wagombea katika nafasi hiyo ya uenyekiti wa baraza la senate walikuwa ni marais saba wa serikali za wanafunzi na zoezi la kuomba kura kwa wajumbe lilitangulia kabla ya uchaguzi kufanyika.

Waliogombea nafasi hiyo ni 

1. Nice Munissy - Rais chuo cha Diplomasia
2. Marwa Wambura - Cardinal Rugambwa Memorial University College - CARUMUCO
3. Eliah Kandonga - Rais Cuhas Bugando
4. Peter Mayunga - Rais wa Chuo cha CBE Dar es salaam
5. Samwel Nyangi - Rais chuo cha Tengeru Institute of Community Development
6. Ernest Kova - Dar es salam Institute of Technology
7. Sylilo Joseph - MUST

Aidha kutokana na kutokuwa na mgombea aliyepata kura zaidi ya asilimia hamsini,  uchaguzi huo ilibidi urudiwe kwa wagombea wawili waliopata kura zaidi ya asilimia kumi na tano, ambao ni Nice Munisy na Peter Mayunga.

Baada ya zoezi la upigaji kura Mheshimiwa Peter Mayunga ndiyo akaibuka mshindi wa nafasi hiyo ya uenyekiti wa baraza la senate TAHLISO kwa kupata asilimia 60.42 ya kura zote.

Wajumbe wa tume ya uchaguzi wakila kiapo kwa pamoja kabla ya kusimamia zoezi la upigaji kura.

Zoezi la kuhesabu kura likiendeshwa kwa umakini

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi na wajumbe wake wakitangaza matokeo ya uchaguzi huo.




Baada ya zoezi la uchaguzi wa mwenyekiti wa baraza la seneti - TAHLISO kumalizika, mwenyekiti wa TAHLISO Mheshimiwa Stanslaus Peter Kadugalize, alitangaza majina ya makamishna wakaoongoza idara zilizomo ndani ya TAHLISO.

Makamisha walioteuliwa na nyadhifa zao katika serikali za wanafunzi na vyuo wanavyotoka ni kama ifuatavyo.

Idara ya Mitaala na Taaluma itaongozwa na kamishna Peninna Moka (Spika - Kampala International University) akisaidiana na Kassim Salim Abdi kutoka Zanzibar.

Idara ya Mikopo, Udahili na Usajili itaongozwa na kamishna Godfrey Martin Joho (Rais wa serikali ya wanafunzi - Tanzania  Institute of Accountancy - DSM)  akisaidiana na Japhet Masatu (Rais wa serikali ya wanafunzi Open University of Tanzania - Kinondoni DSM).

Idara ya Habari na Mawasiliano - Kamishna wake ni Hemed Haroub (Rais  Institute of Social Work - DSM), akisaidiana na Aivan Maganza (Rais wa serikali ya wanafunzi St. Joseph University - DAR).

Idara ya Michezo na Ziara mbalimbali - Kamishna wake ni Mkumbo Iman (Rais wa serikali ya wanafunzi Institute of Accountancy Arusha - IAA) na George Albert Mnali (Rais wa serikali ya wanafunzi - Dar es salaam Maritime Institute).

Idara ya Mahusiano, Mihadhara na Makongamano - Kamishna wake ni Thomas Jackson Shauri (Rais wa serikali ya wanafunzi - Hubert Kairuki Memorial University) akisaidiana na Mende Tito (Makamu wa Rais wa serikali ya wanafunzi STEMMUCO - Mtwara).

Idara ya Mahafali na Maafa - Kamishna wake ni Neema Lelisha (Makamu wa rais wa serikali ya wanafunzi ST. John Dodoma) akisaidiana na Manusura Lusigaliye (Rais wa serikali ya wanafunzi CBE - Lake Zone).

Idara ya Uchumi - itaongozwa na Kamishna Asha Feruzi (Spika wa bunge la serikali ya wanafunzi - Institute of Adult Education) akisaidiana na Marwa Charles (Rais wa serikali ya wanafunzi - Jordan University - Morogoro).











Wajumbe wa baraza la Seneti - TAHLISO kwa wakifuatilia kwa umakini mkutano wa baraza hilo.





Continue Reading...
Continue Reading...

MARAIS WA SERIKALI ZA WANAFUNZI VYUO VIKUU NCHINI - TAHLISO WAKUTANA KATIKA CHUO CHA USTAWI WA JAMII KWA AJILI YA UCHAGUZI WA VIONGOZI WA TAHLISO.

Baraza kuu la viongozi wa serikali ya wanafunzi ya vyuo vikuu nchini, Tanzania Higher Learning Institute Students Organisation - TAHLISO, linalohusisha marais wa vyuo, limekutana katika chuo cha ustawi wa jamii, kwa ajili ya uchaguzi wa viongozi wa Taasisi hiyo.







Viongozi wanaowakikisha serikali za wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali nchini, waliohudhuria mkutano huo wa uchaguzi.

Kabla ya uchaguzi, mkutano huo ulianza kwa kuwapata wajumbe wa tume ya uchaguzi watakaosimamia uchaguzi huo.

Wajumbe wa tume ya uchaguzi, wakila kipo cha kusimamia uchaguzi kwa uadilifu.  

Mkutano huo umehudhuriwa na marais wanaoongoza serikali za wanafunzi kutoka vyuo thelathini na sita (36) Tanzania Bara na Visiwani.
Continue Reading...

Followers

Check us on Facebook

Designed By WijasWillie | SharpMedia