Wednesday, 30 November 2016

Mkutano Mkuu wa Wanafunzi Tarehe 30 Nov 2016 Ulikua Hivi

Mhe Erasto Nassary
Waziri Ofisi ya Rais Usalama na Itifaki
Muda wa Kuingia kwa Mhe Rais, Makamu wa Rais Pamoja na Waziri Mkuu

 Kutoka Kushoto ni Waziri Wa Elimu Mhe Fadhili, akiteta jambo na Mhe Hellen (Makamu wa Rais) kabla ya Mkutano Kuanza Kuanzia hapo Kilia ni Mhe Rais Mhe Yohana Mabena na mwisho kulia ni Waziri Mkuu Mhe Godfrey
 Baadhi ya Wajumbe (wanafunzi) wakisikiliza

 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Moses Mvuoni akidadavua kitu kuhusiana na Katiba
 Makamu wa Rais Akiongea machache


 Wanafunzi walijaa hadi wengine Kusimama

 Mhe Rais Akitoa Hotuba Yake

 Maswali yaliulizwa 


 Mhe Nassoro Mbunge BHRM2A

Hakika Umakini na Usikivu ulitawala



Karibuni katika SGM nyingine imeletwa kwako na Wizara ya Habari
Continue Reading...

Friday, 4 November 2016

Matukio ya Siku ya Kikao cha Rais na Mawaziri wake

 Mhe Rais na Mhe Makamu wa Rais katika Kikao cha Dharura kilichofanyika mnamo tarehe 28 Oct na Baraza la Mawaziri



  
Mhe Emmanuel Laizer
Waziri wa Fedha

Mhe Silver Ngaiza
Naibu Waziri wa Mipango na Uchumi

 Mhe Boniface Daudi
Naibu Waziri wa Mikopo

Mhe Ericky Maghembe
Naibu Waziri wa Makazi na Ulinzi

 Wizara ya Michezo kutoka kushoto nyuma ni Mhe Evance Mushi Waziri wa Michezo na Burudani, katikati Mhe Saad Chande Naibu Waziri wa Michezo na Burudani mbele kulia ni Mhe Ashura Jingu Naibu Waziri wa Michezo

Continue Reading...

Tuesday, 18 October 2016

MAJINA YA WANAFUNZI WALOCHAGULIWA USTAWI HAYA HAPA


Kutazama majina hayo pitia link hii hapa then utaenda mahala pameandikwa download then click hapo na utaona hapo... BOFYA HAPA
Continue Reading...

Friday, 14 October 2016

TAZAMA HAPA STRUCTURE MPYA YA ADA, NA HOSTELI MWAKA wa Masomo 2016/2017

Ada mpya kwa wanafunzi wa mwaka wakwanza pia Hosteli itakua kwa Wote...Mtaarifu na Mwenzio aone mchanganuo huo
Continue Reading...

Wednesday, 31 August 2016

Ratiba ya Mitihani ya Sap/ Special examz

 
Wizara ya Elimu ISWOSO inapenda kuwatangazia kuwa 
Mitihani ya special, deffered na supplementary ya muhula Wa pili
inatarajiwa kuanza mnamo 
tarehe 14/9/2016 na kumalizika tarehe 23/9/2016.

Wizara zinapenda kuwakumbusha kujiandaa vyema na 
kuwatakia maandalizi mema kwa wote
wanatarajiwa kufanya mitihani hiyo.
 
 
kwa Taarifa za papo kwa Papo  ndani ya USTAWI basi download APP ya LAA
ndani ya Playstore
 
                          
Continue Reading...

Tambua haki yako ya kuappeal..

 


WIZARA YA ELIMU KWA KUSHIRIKIANA NA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA.

Inapenda kuwakumbusha wale wote  waliokwisha pata matokeo yao ya muhula Wa pili Wa masomo na wana uhitaji kwa kukata rufaa ,Kwamba kwa mujibu Wa prospectus 2015/16 Almanac ya Taaluma mwaka 2015/16  rufaa zote kuhusiana na matokeo ya mtihani zitapokelewa katika ofisi ya makamu mkuu Wa chuo ,Taaluma,utafiti na ushauri Wa kitaaluma kuanzia tarehe 30/8/2016 hadi tarehe 2/9/2016, gharama ni  shilingi elfu arobaini(40,000) kwa kila somo litakalo katiwa rufaa.

NB:Rufaa zote zitakazowasilishwa  nje ya muda hazitasikilizwa hivyo ni muhimu na Lazima kuwasilisha ndani ya Muda stahiki.

Kwa mawasiliano zaidi;
Waziri Wa Elimu               0715370377
Waziri katiba na sheria      0718535614
Naibu waziri elimu            0767561466
Naibu waziri Elimu            0659187166
Naibu waziri katiba na sheria-0712527041
Continue Reading...

Friday, 13 May 2016

PATA VIONJO - YALIYOJIRI KWENYE CAREER DAY USTAWI WA JAMII

Katika kunogesha maadhimisho ya siku ya ujuzi (Career day) yaliyofanyika jana alhamisi ya tarehe 12/05/2016, vikundi mbalimbali vya kitaaluma vilitoa burudani inayohusiana na kile wanachojifunza katika taaluma yao.

Kwa upande wa taaluma ya Social work, wanaharakati wa kikundi cha Protect Her 4 Life, chenye lengo la kupambana na kila aina ya ukatili wanaofanyiwa wanawake na wasichana, kilitoa igizo lililolenga namna ukatili unavyofanyika, ni kwa kiasi gani kutojielewa au kutojengewa uwezo kunavyosababisha mtu kutoweza kushiriki katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo, namna mwanamume anayomtupia lawama mke kwa kila tatizo linalomkuta mtoto na kuelimishwa kuwa naye anapaswa kuwa sehemu ya kutoa malezi bora kwa watoto.

Pia igizo hilo lilionesha ni kwa namna gani afisa ustawi wa jamii anavyoweza kufanya kazi na timu ya wataalamu wa fani mbalimbali, na katika igizo hili wameshirikiana na polisi kufanikisha mwanamume aliyefanya ukatili amekamatwa na kufikishwa dawati la jinsia, pia afisa ustawi wa jamii ameweza kushirikiana na mwalimu wa shule katika kusaidiana kutoa elimu ya afya ya uzazi kwa vijana hasa kipindi cha balehe ili kuepuka mimba wakiwa mashuleni na kuonesha ni kwa kiasi gani maafisa ustawi wa jamii wahahitajika mashuleni. Na pia kumjengea uwezo mwanamke afahamu haki zake na fursa mbalimbali za kimaendeleo.



Wanachuo wa fani ya ustawi wakijiandaa kwa igizo

Mwanamke aliyepigwa na mumewe akishauriwa kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi, kutokana na kipigo cha mara kwa mara anachokipata kwa mumewe.





Msoma risala kwa upande wa Industrial Relations wao hawakuwa na igizo.





Continue Reading...

Thursday, 12 May 2016

CAREER DAY 2016 YAFANA USTAWI WA JAMII


Kilele cha maadhimisho ya ujuzi (Career day) katika chuo cha ustawi wa jamii, kimehitimishwa leo katika viwanja vya chuo cha ustawi wa jamii – Dar es Salaam.



Baadhi ya wanachuo wa taaluma ya ustawi wa jamii waliohudhuria maadhimisho hayo


Baadhi ya wanachuo wa taaluma ya Industrial Relation waliohudhuria maadhimisho hayo


Baadhi ya wanachuo wa taaluma ya Human Resource waliohudhuria maadhimisho hayo


Akitoa salamu za ufunguzi, rais wa serikali ya wanafunzi chuo cha ustawi wa jamii Mheshimiwa Hemed Haroub, amebainisha kuwa siku hii inalenga kuwakutanisha pamoja wajuzi wa fani zinazotolewa katika chuo cha ustawi wa jamii, pamoja na wale walio katika ajira, katika kushea mambo mbalimbali, na pia kutoa mawazo ya fursa za ajira.


Mheshimiwa Hemed - rais wa serikali ya wanafunzi


Rais wa serikali ya wanafunzi Mheshimiwa Hemed Haroub (aliyesimama) akitambulisha meza kuu, wa kwanza kulia ni makamu wa rais wa serikali ya wanafunzi chuoni hapo Mheshimiwa Stella Wadson


Kilele cha maadhimisho hayo kimefana kwa wanachuo kuainisha shughuli mbalimbali zinazofanywa na taaluma zao kwa njia ya maelezo, maigizo na kupitia risala.







 Pichani juu ni wanachuo wa taaluma ya ustawi wa jamii, wakielezea mambo mambo mbalimbali wanayofundishwa katika taaluma hiyo na namna inavyowasaidia katika kufanya kazi mbalimbali za kijamii.




Pichani ni wanataaluma ya Industrial Relation wakielezea shughuli zinazotekelezwa na wanataaluma hiyo pamoja na process nzima inavyotakiwa kufuatwa wakati wa kufanya Mediation.




Hapa ni kwenye meza ya wanachuo wa taaluma ya rasilimali watu (Human Resource) nao wakielezea kile wanachokipata katika chuo cha ustawi wa jamii, pamoja na namna taaluma hiyo inavyofanya kazi kwenye soko la ajira.


Wawakilishi kutoka mashirika mbalimbali waliweza kuhudhuria katika career day ya ustawi wa jamii, kutoa changamoto mbalimbali zinazotokana na ajira na pia kutoa mwongozo wa namna ya kuchangamkia fursa mbalimbali za ajira.

Miongoni mwa mashirika na wadau waliohudhuria ni pamoja Brighter Monday, PSPF, Zoom Tanzania pamoja na wawakilishi wa vyuo mbalimbali kikiwemo chuo kikuu cha Dar es Salaam.


Mwakilishi kutoka Brighter Monday, akielezea fursa mbalimbali za ajira zinazopatikana endapo mtu atajiunga online ili kupata taarifa mbalimbali za nafasi za ajira hapa nchini, kutoka kwa mashirika mbalimbali.


Career day katika ustawi wa jamii imeandaliwa na wizara ya elimu kutoka serikali ya wanafunzi ISWOSO kwa kushirikiana vilabu vya kila taaluma itolewayo ambapo kwa upande wa Human Resource inafahamika kama IHUMRESA, Industrial Relations – IRESA na Social Work – SOWOC.
Waziri wa elimu katika serikali ya wanafunzi - ISWOSO Mheshimiwa Mabena, akihojiwa na chombo cha habari cha ITV, kuelezea lengo la career day.










 Pichani juu ni baadhi ya wanachuo waliohudhuria kwenye career day, iliyofanyika katika viwanja vya chuo cha ustawi wa jamii.

Maadhimisho ya career day hufanyika kila mwaka na kwa kipindi yamehusisha taaluma zote tatu zinazotolewa katika chuo cha ustawi wa jamii ambazo ni Social work, Human Resource, na Industrial Relations, lengo likiwa ni kuziweka pamoja na kuongeza ufanisi, kwani hata katika soko la ajira zinategemeana, tofauti na miaka ya nyuma ambapo kila taaluma ilikuwa inaadhisha kivyake.

Continue Reading...

Followers

Check us on Facebook

Designed By WijasWillie | SharpMedia