Pichani ni Waziri wa Miundombinu ISWOSO 2016/2016 Mh. Erasto Nassary, akionesha sehemu ya vitendea kazi vinavyoendea kutengenezwa kwa ajili ya ujenzi wa vimbweta vipya. (picha zote ni kwa hisani ya wizara ya habari ISWOSO)
Ili kufanikisha suala hilo, wizara ya miundombinu katika serikali ya wanafunzi ISWOSO 2015/2016, imejipanga kuongeza idadi ya vimbweta zaidi ya ishirini baada ya jitihada za kupata ufadhili wa kufanikisha suala hilo kutoka asasi mbalimbali, huku kampuni ya mawasiliano ya ZANTEL ikitoa mchango wake wa miamvuli 70 iliyoanza kuwekwa kwenye vimbweta vya awali ili wanafunzi waweze kujikinga na jua.
Pichani ni fundi akiendelea na maandalizi ya utengenezaji wa vimbweta vipya.
Pichani juu ni baadhi ya vimbweta vya zamani vikiwa vimewekwa miamvuli iliyotolewa na Zantel kwa ajili ya kuwezesha wanafunzi kujikinga kipindi cha jua na manyunyu wakati wakijisomea.
Waziri wa Miundombinu ISWOSO 2015/2016 Mh. Nassary akiwa kwenye moja ya vimbweta vya awali vilivyowekwa miamvuli kwa hisani ya kampuni ya mawasiliano ya ZANTEL.
Mh. Nassari, amebainisha kuwa vimbweta vinavyotarajiwa kutengenezwa vitakuwa kwa mtindo wa duara ili kuendana na sawa na umbo la miamvuli hiyo, na amewataka wanafunzi kutoondoa miamvuli hiyo sehemu ilipo na endapo atakaa kwenye kimbweta ambacho hakina mwamvuli afike ofisi za ISWOSO na kuelezea suala hilo kwani miamvuli mingine imehifadhiwa ofisini na si kuhamisha iliyowekwa kwenye vimbweta vingine.
NB: Shukran kwa kampuni ya Mawasiliano ya ZANTEL kwa msaada wa miamvuli